Short stories from members who chose to share how God answered prayer. Your own prayer requests stay private unless you publish a testimony here.
kuanzisha biashara
Ninamshukuru Mungu sana tena alsana maana sabuni ambayo nilitengeneza ya kwanza wateja waliyinunuwa na nikapata faida.
Pastor Mungu amenitendeya makubwa mengi siwezi kunyamanza.Mungu hujibu maombi jamani.
Asante sana mchungaji Mungu akubariki na akupe afiya njema.
namshukuru Mungu maana kweli ufaulu wa watoto wangu uko juu mno jina la Mungu litukuzwe sana
Ninamshukuru Mungu wa mbinguni Pr siku ya tarehe 09/07 mwaka huu. niliota ndoto nikiwa nimelala mchana kwamba tulikuwa na wewe kwenye kambi fulani. nikapata nafasi ya kuongea na wewe kitu ambacho ulinambia ni kwamba Kuna kitu kizuri Mungu ameweka ndani ya kinywa changu.. na baada ya mda mchache ukaniuliza tena umenielewa nikajibu nikasema nitaifanya kazi ya Mungu endapo Mungu ataniongoza ukaniambia hicho ndipo ninapaswa kuomba. kiukweli Pr. ndani yangu ninajua nina wito katika kazi ya Mungu lakini sielewi nifanye nini ili Mungu anipatie Mwongozo. ndani yangu Pastor ninahisi kuna nguvu za giza huu ni mwaka wa 4 sasa na sijui nifanye nini mpaka sasa. Naomba unisaidie katika hili.
ni mkuu na anatend
Ndoa
Bwana yesu asifiwe, nashukuru Mungu kwa kuniombea ombi langu, mke nilioa aliyenitoroka Bado hajarudi tunawasiliana tu, kaniambia nioe mwanamke mwingine,
1.Mungu anaendelea kumpigania babu yangu anaendelea vizuri.
2.Mungu anatusaidia katika masomo yetu sana.
3.Nimetambua kusudi la maisha yangu, naomba Mungu anisaidie kulitimiza.
Familia yangu
Hali ya sasa ya baba na mama sii kama hapo awali sahiv baba anazungumza angalau na kuelewana na mama,naamin mungu anazid kujibu
MUNGU AMENIFUNGUA KIFUNGO NA SASA NIPO HURU. NAMSHUKUR BABA WA MBINGUNI KWA KUWA ANASIKIA, NILIFUNGWA NA GIZA ILA SASA NAANZA KUONA NURU NA AFYA YANGU IMEANZA KUREJEA
NA BWANA ATAZIDI KUNIANGAZIA NURU YAKE KWA KADIRI YA WINGI WA NEEMA YAKE🙏
Bwana yesu asifiwe!! Nina mushukuru Mungu sana kwa matendo makubwa anayo tenda kila siku ndani ya maisha yetu mimi n'a jamaa langu. leo nyumba ya kaka yangu imeungua wakati yupo safari n'a mke wake, Mungu asifiwe kwa sababu moto huo hawakuuona n'a wala hauku wazuru. pengine tungeongea habari nyengine leo. sofa zimurudie Mungu mkuu sana.Nina mushukuru tena Mungu kwaku nipa baraka zake, na kuniongoza kila siku. nilikua n'a tabia ya kuiba ila Mungu amanisaidia mpaka nashangaa nimeacha kuiba, kwa hili nasifu Mungu sana. ni mimi Rachel kutoka congo
kiukweli sikio langu bando halisikii na sijui kwa nini ila naamini ipo siku litasikia tena.
UPONYAJI WA ETHAN MWANANGU
Napenda kumshukuru Mungu kwaajili ya uponyaji wa mtoto wangu Ethan Josephat kwasasa anaendelea vizur anakula vizuri hakika Mungu ni mkubwa mno